Episodes
Wednesday Jul 15, 2020
Nidhamu za Kiroho 2: Utunze Hali Yako ya Kiroho
Wednesday Jul 15, 2020
Wednesday Jul 15, 2020
Adui wetu hufurahi sana akiona kiongozi anayeacha nidhamu za msingi za kiroho na kuanza kujitegemea nguvu zake na hekima yake. Katika podcast hii tunaendelea na maongezi yetu na Mzee Vernon Smith juu ya maisha ya kiroho ya kiongozi. Mgeni wetu anatupa mashauri mazuri juu ya utunzaji wa hali yetu ya kiroho na umuhimu wa kutembea na Yesu kwa karibu siku zote.
Tuesday Jun 30, 2020
Nidhamu za Kiroho 1: Maisha ya Kibinafsi ya Kiongozi
Tuesday Jun 30, 2020
Tuesday Jun 30, 2020
Mzee Vernon Smith yuko nasi katika podcast hii, akijibu maswali yangu juu ya Nidhamu za Kiroho katika maisha ya kiongozi. Katika podcast hii ya kwanza anatoa ushauri wake juu ya mambo ya lazima yaliyopaswa kuwemo katika maisha ya kiongozi wa kiroho ili adumu katika huduma na awe na ushuhuda mwema kama mtu wa Mungu.
Monday Jun 15, 2020
Kiongozi Katika Jamii: Kinachoathiri Jamii Yetu
Monday Jun 15, 2020
Monday Jun 15, 2020
Ni nini inayoweza kubadilisha maisha ya watu na kuleta athari katika jamii? Ni Neno la Mungu. Mgeni wetu, Mchungaji Ngunjiri, anatoa mashauri juu ya nguvu ya Neno kubadili maisha ya watu na tunasihiwa kupanda Neno la Mungu katika huduma zetu na kumwachia Bwana afanye kazi na kuleta matunda kupitia Roho wake na Neno lake.
Saturday May 30, 2020
Kiongozi Katika Jamii: Huduma Yenye Maana
Saturday May 30, 2020
Saturday May 30, 2020
Huduma ya kiongozi inaweza kuwa na nguvu na kutumiwa na Bwana kuathiri jamii yake. Mchungaji Ngunjiri anasisitiza umuhimu wa kiongozi kushirikiana vizuri na majirani na watu wa eneo lake, na kuandaa huduma ambazo zinabariki jamii na kuwasaidia katika maisha yao ya kila siku. Kwa njia hiyo, Neno la Mungu linahubiriwa na watu wanaguswa.
Friday May 15, 2020
Kiongozi Katika Jamii: Ushuhuda wa Familia
Friday May 15, 2020
Friday May 15, 2020
Mchungaji Stephen Ngunjiri anaeleza umuhimu wa kiongozi wa kiroho kuwa na sifa njema na ushuhuda mzuri katika jamii, na sio tu ushuhuda wake bali ni ushuhuda wa mkewe na watoto wake pia.
Thursday Apr 30, 2020
Kukabidhi Wengine Huduma Kwa Mafanikio
Thursday Apr 30, 2020
Thursday Apr 30, 2020
Tusipotumia hekima katika ugawaji wa huduma, badala ya kuona baraka na huduma kusonga mbele, tunaweza kujuta kwa nini nilimpa mtu fulani kazi. Katika episode hii ya mwisho katika mfululizo huu, kuna ushauri kuhusu kukabidhi wengine huduma kwa njia ambayo huleta mafanikio katika huduma na upevu katika maisha ya viongozi wa baadaye.
Friday Apr 10, 2020
COVID 19 na Wewe
Friday Apr 10, 2020
Friday Apr 10, 2020
Daktari Robert Byemba ana mashauri kwa ajili yetu kuhusu virusi vya Korona (COVID 19) na kuhusu wajibu wetu kama viongozi wa kiroho. Sio wakati wa kuogopa na kuacha kufanya huduma, bali ni wakati wa kuchukua fursa ya hudumia wengine kwa ujasiri.
Tuesday Mar 31, 2020
Kwa Njia Gani Nianze?
Tuesday Mar 31, 2020
Tuesday Mar 31, 2020
Uko tayari kushiriki mzigo wa huduma na wengine na kuwakabidhi wengine kazi. Unaanzaje? Katika episode hii tunajifunza hatua kwa hatua jinsi ya kuwashirikisha wengine katika huduma.
Friday Mar 20, 2020
Jibu Letu Wakati wa Janga
Friday Mar 20, 2020
Friday Mar 20, 2020
Tunaishi katika wakati ambao ulimwengu haujawahi kuona. Watu wako katika hali ya woga na mashaka kutokana na virusi vya Korona 19. Kama viongozi wa kiroho, je, tunapaswa kujibu namna gani? Je, Mimi na wewe tunatakiwa kuishi namna gani katika wakati huu wa historia?
Saturday Feb 29, 2020
Kwa Nini Hatushiriki Kazi?
Saturday Feb 29, 2020
Saturday Feb 29, 2020
Kabla ya kujifunza kwa njia gani tunaweza kuwagawia wengine huduma, ni bora kuangalia sababu mbalimbali kwa nini viongozi wengine wanaona ni vigumu kuwashirikisha wengine kazi.