Episodes

Wednesday Oct 27, 2021
Sifa za Kiongozi 3 - Fedha ya Aibu
Wednesday Oct 27, 2021
Wednesday Oct 27, 2021
Kila kiongozi wa kiroho anapaswa kujiuliza swali: “Kwa nini ninamtumikia Bwana?” Amini, usiamini, kuna viongozi wengi ambao wamesahau wito wao na maana yake na wameanza kufanya huduma kwa ajili ya mapato. Katika podcast hii tutaangalia Neno la Mungu kwa viongozi kupitia waraka wa Paulo kwa Timotheo. Je, unatamani fedha ya aibu?

Thursday Sep 02, 2021
Sifa za Kiongozi 2 - Kauli Moja
Thursday Sep 02, 2021
Thursday Sep 02, 2021
Katika podcast hii tunaendelea kukazia sifa muhimu za Kiongozi wa Kiroho. Lazima atawale ulimi wake na kutunza maneno yake na asiwe mtu wa kusengenya watu. Kiongozi awe mtu anayesema wazi, bila kuficha ficha maana yake, na asiwe mtu wa kuwasema watu wengine.

Monday Aug 02, 2021
Maisha ya Umisionari
Monday Aug 02, 2021
Monday Aug 02, 2021
Mmisionari ambaye amekubali wito wa Bwana na kutumwa kwa watu wa lugha na utamaduni tofauti hupaswa kuzoea maisha mapya. Kuna changamoto nyingi, lakini pia kuna baraka kwa sababu ya kutii sauti ya Bwana na kumtegemea Yeye aliyemwita. Katika podcast hii tunaendelea na maongezi yetu na Mmisionari Daudi Likama na kusikia ushuhuda wake juu ya maisha na huduma yake Msumbiji. Bwana atumie ushuhuda wake ili kutuhimiza sisi sote na kufanya masikio yetu tayari kusikia wito wa Bwana kwa ajili yetu.

Friday Jul 02, 2021
Kuitikia Wito wa Umisionari
Friday Jul 02, 2021
Friday Jul 02, 2021
Wengi walisema “haiwezekani!” Walidai kwamba Tanzania ni nchi maskini na kuna haja ya wamisionari kuja Tanzania na kuleta Injili. Lakini Mmisionari Mtanzania kutumwa na kanisa la Tanzania na kupeleka Injili nje si rahisi. Lakini Bwana aliita na Ndugu Likama aliitika. Jiunga nasi katika podcast hii na ijayo ili kusikia ushuhuda wa Ndugu Daudi Likama aliyetumwa na kanisa lake kupeleka habari njema ya wokovu Msumbiji.

Monday Feb 15, 2021
Sifa za Kiongozi 1- Msimamo
Monday Feb 15, 2021
Monday Feb 15, 2021
Walio viongozi kweli kweli si viongozi wa jina tu, bali ni viongozi waliostahili kuongoza kutokana na msimamo wao na uaminifu wao mbele za Mungu na mbele ya watu. Katika podcast hii ya na podcast zifuatazo tutaangalia sifa za muhimu ambazo humfanya mtu awe kiongozi mwaminifu aliyetumiwa na Bwana kuongoza wengine vema.

Saturday Jan 30, 2021
Hekima Kutoka Kwa Kiongozi Mwanamke
Saturday Jan 30, 2021
Saturday Jan 30, 2021
Sikiliza mashauri na hekima ya mwanamke mwaminifu ambaye amekuwa kiongozi wa kiroho siku nyingi. Katika podcast hii tunamwuliza juu ya familia yake, huduma yake, baraka na changamoto anazoziona katika uongozi wake n.k. Podcast hii si tu kwa ajili ya akina dada. Kiongozi mwanamume, sisi pia tunahitaji hekima hii kutoka kwa Mama Moses. Karibu tusikilize!

Friday Jan 15, 2021
Ubora wa Viongozi Wanawake
Friday Jan 15, 2021
Friday Jan 15, 2021
Je, ni lazima mwanamke awe nyuma ya mwanamume katika ulimwengu wa uongozi? Wanawake wanafaa tu kusaidia waume zao na wanaume wengine, au wanawake wanafaa kuongoza wenyewe katika mambo ya kiroho? Katika podcast hii tunaongea na wanawake waaminifu walio viongozi wenyewe. Ni wake wa wachungaji na wasaidizi wa waume zao katika huduma. Lakini hawa wanawake ni zaidi ya wasaidizi. Wenyewe wanaongoza katika huduma na wao wenyewe ni viongozi katika mambo ya kiroho.

Friday Jan 01, 2021
Tafakari Njia Yako
Friday Jan 01, 2021
Friday Jan 01, 2021
Heri ya Mwaka Mpya! Siku za kwanza za mwaka mpya ni wakati mzuri wa kutathmini juu ya maisha yetu, huduma yetu, na hali yetu ya kiroho kama viongozi. Podcast hii ni ujumbe maalum nilioandaa kwa ajili yako tunapoanza mwaka 2021. Kama umeanza kuchoka, kushuka moyo, au kukosa maono katika huduma, naomba usikilize podcast hii na kutiwa moyo. Tutaangalia mfano wa watu wa Mungu waliochoka na kupoteza furaha katika huduma, lakini kupitia ujumbe wa nabii wa Mungu walisaidiwa sana na hatimaye kuona mafanikio, ridhaa, na furaha katika huduma yao mbele za Bwana.

Monday Nov 30, 2020
Kiongozi na Timu Yake 2
Monday Nov 30, 2020
Monday Nov 30, 2020
Si watu wote wanaofaa kufanya huduma katika timu. Kiongozi lazima awe na tabia fulani na wanatimu pia wawe watu wa namna ya pekee. Sikiliza podcast hii tunapoendelea na mada ya "timu" na kuzungumzia ubora wa kufanya huduma pamoja na watu wengine wanaofaa.

Sunday Nov 15, 2020
Kiongozi na Timu Yake 1
Sunday Nov 15, 2020
Sunday Nov 15, 2020
Mhubiri alisema, "Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; kwa sababu wana tuzo njema kwa kazi yao." (Mhubiri 4:9). Katika podcast hii na podcast ijayo tutasikia kutoka kwa kiongozi wa kiroho ambaye amekuwa akiongoza timu katika huduma siku nyingi, katika mahali ambapo ardhi ni ngumu na nguvu ya timu ni muhimu. Anatushauri namna gani tunaweza kuwekeza katika watu wengine na kuona manufaa na matunda kwa kufanya huduma pamoja.